Skip to main content

WANANDOA MPOOO?? NISIKILIZENI KWA MAKINI WANANDOA.

1.UTAMSHANGAA SANA:
Image may contain: one or more people, ocean, beach, water, shoes, sky, outdoor and nature
Mnapooana, hasa baada ya kumpata yule unadhani ni mwenzi halisi na anayekufaa unaamini kwamba utakuwa naye kwa furaha hadi kifo kitakapo watenganisha na utakuwa mtu wa furaha milele.
Ila siku moja utaamka asubuhi na kugundua kwamba hata kama ni mtu maarufu sana duniani bado hawezi kukufanya wewe kuwa mtu wa furaha siku zote na zipo siku utakuwa uajiuliza hivi kwa nini ulikuwa na haraka kumkubali na kuoana naye.
Sasa matarajio yanapotea, unajisikia upweke, na unaaanza kujifunza kwamba ndoa si kituo kufikia baada ya maisha ya kujitafutia mtu wa kuishi naye duniani bali safari iliyojaa raha na karaha kuelekea kujuana na kujenga familia bora na imara.
2.UTAFANYA KAZI KUBWA ZAIDI YA ULIVYOTEGEMEA.
Mapema watu wanapokwambia ndoa ni kazi unadhani labda itakuwa ni kuvumilia kwa kuwa mwenzako anasahau kufanya wajibu wake katika kazi za kila siku ndani ya nyumba.
Na unaamini kwamba hata kama anatabia fulani fulani mbaya basi utamvumilia kwa kuwa unampenda.
Kuoana ni kudhihirisa umemaliza degree ya kwanza sasa unaingia Graduate studies (Masters au Phd) na inahitaji kazi kuliko unavyotegemea.
Ndiyo maana sasa unapambana na matatizo hayo unayopitia kwani inawezekana hukudhani kwamba siku moja utajikuta katika njia panda ambayo unahisi inakuchanganya zaidi.
Hata hivyo bado nafasi unayo na ndoa yako ina uhai mkubwa
3.KUNA WAKATI UTAENDA KULALA OVYO KABISA
Wengi huwashauri wanandoa wapya kwamba “usiende kulala huku umekasirika” kama vile hawajui nini hutokea kwenye vyumba vya kulala vya wanandoa.
Na wengine hujihurumia sana kwa kuwa wapo single eti usingizi ni wa mang'amung'amu wakioa na kuolewa ndipo watalala vizuri vifuani mwa wapenzi wao.
Thubutu! vyumba vingine vya kulala ni kisima cha machozi na kelele za migogoro hadi usiku wa manane hata usingizi hakuna.
Kitu cha msingi ukikasirishwa just come down and be loving endelea na maisha hakuna mtu anaweza kukufanya uwe na furaha isipokwa wewe kwanza..
4.KUNA WAKATI UTAISHI BILA TENDO LA NDOA
Si kwamba siku zote wanandoa huwa na mood kwa ajili ya sex, anaweza kuwa mmoja au wote. Kukosa mood au sex drive ni sehemu ya maisha ya ndoa na hii haina maana kwamba hutataka sex tena bali ni kipindi kutokana na maisha yanavyoenda.
Kitu cha msingi ni kwamba hata kama hamfanyi basi kunatakiwa kuwepo na romantic life kama vile touching, kissing, hugging.
Hivyo ingia kwenye ndoa ukijua sex si chakula bali hitaji la mwili kwa ajili ya kuridhishana wawili wanaoishi pamoja.
5.NDOA IMARA HAINA MAANA HAKUNA MIGOGORO
Kubishana au kupingana au kupishana kimawazo au jambo lolote ni sehemu ya maisha ya ndoa.
Pia ni njia nzuri ya kujuana na kuwekana sawa tena hili inabidi lifanywe kwa upendo pia kuvumiliana na kuyamaliza ndani ya dakika 15

Comments

Popular posts from this blog

MKE MWEMA MTU HUPEWA NA BWANA. SIFA ZA MKE MWEMA

SIFA ZA MKE MWEMA 1) Kamwe usinyanyue sauti yako kwa mumeo kwa sababu yoyote ile. Hiyo ni ishara kuwa huna adabu na heshima. Pia niliwahi kufundisha hapa Ndoa Maridhawa kuwa radi haioteshi mazao yetu shambani licha ya kuwa na kelele na sauti kubwa, lakini mvua ambayo haina makelele huotesha mazao yetu shambani. 2) Usitangaze udhaifu wa mumeo kwa familia yako na marafiki zako. Linaweza kukuathiri wewe pia. Wewe ni mtunza siri wa mwenzako, na yeye ni mtunza siri wako. 3) Usitumie mihemko na hisia kali kuwasiliana na mumeo, hujui namna atakavyoitafsiri. Wanawake wenye mihemko iliyopitiliza hawawezi kuwa na ndoa yenye furaha. 4) Usimlinganishe mumeo na wanaume wengine, hujui undani wa maisha ya hao wengine. Ukiishambulia HADHI yake, upendo wake kwako utayeyuka. 5) Usiamiliane vibaya na marafiki wa mumeo kwa sababu tu huwapendi, mtu anayepaswa kuepukana nao ni mumeo. 6) Usisahay kuwa mumeo alikuoa wewe, hakumuoa huyo mfanyakazi wako wa ndani au mtu mwingine. Fany...

Vidokezo 10 vya kufurahia barbeque au pikiniki wakati wa ujauzito

Hapa kuna vidokezo kadhaa vya kufanya pikiniki au BBQ zifanyie kazi wakati ukiwa ni mjamzito 1. Jua ni vyakula vipi vya kuzuia ukiwa mjamzito. Bado unaweza kufurahiya vyakula vingi lakini vyakula muhimu vya msimu wa joto ambavyo unapaswa kujiepusha ni pamoja na: jibini laini lisilopikwa, kuponya nyama, mayonnaise ya nyumbani isipokuwa imetengenezwa na mayai makubwa ya simba (mayonesi iliyonunuliwa duka ni sawa), ice cream ya nyumbani isipokuwa imetengenezwa na mayai makubwa ya simba (tena, barafu-iliyonunuliwa duka ni sawa). 2. Angalia nyama iliyochongwa na samaki . Ni sawa kabisa kumdhihaki Burger kwenye barbeque wakati una mjamzito, lakini angalia ikiwa nyama imepikwa vizuri. Vinginevyo, unaweza kupata sumu ya chakula kutoka kwa bakteria. Angalia kuwa nyama iliyo katikati ni nyekundu na weka skewer kwenye sehemu nene ya nyama ili kuhakikisha juisi iko wazi. Na usijali kuhusu kumkosea mmiliki kwa kuangalia: ni muhimu wakati wewe ni mjamzito. Ikiwa utatengeneza barbeque yako m...
Start a journey to a slimmer, healthier you. This effective, easy-to-follow cleansing program will give you the tools you need to start transforming your body today. Over the next 9 days, you can expect to look better and feel better and begin to eliminate stored toxins that may be keeping you from absorbing the maximum nutrients in your food. You’ll also begin to feel lighter and more energized as you prove you can take control of your appetite and see your body begin to change. Welcome and congratulations for taking charge of your health. I salute you! Your transformation has just began. Am proud and excited for you!? Clean 9 (C9) is a 9 day cleansing phase which is part of the Fit programme from Forever Living Products (USA) which has been here since 1978 giving amazing, highly effective and internationally used health beauty and wellness solutions in over 160 countries worldwide. We give 100% guarantee to our clients as our products speak for themselves with highly recognize...