Skip to main content

MKE MWEMA MTU HUPEWA NA BWANA. SIFA ZA MKE MWEMA



SIFA ZA MKE MWEMA
Image may contain: 1 person, standing
1) Kamwe usinyanyue sauti yako kwa mumeo kwa sababu yoyote ile. Hiyo ni ishara kuwa huna adabu na heshima. Pia niliwahi kufundisha hapa Ndoa Maridhawa kuwa radi haioteshi mazao yetu shambani licha ya kuwa na kelele na sauti kubwa, lakini mvua ambayo haina makelele huotesha mazao yetu shambani.
2) Usitangaze udhaifu wa mumeo kwa familia yako na marafiki zako. Linaweza kukuathiri wewe pia. Wewe ni mtunza siri wa mwenzako, na yeye ni mtunza siri wako.
3) Usitumie mihemko na hisia kali kuwasiliana na mumeo, hujui namna atakavyoitafsiri. Wanawake wenye mihemko iliyopitiliza hawawezi kuwa na ndoa yenye furaha.
4) Usimlinganishe mumeo na wanaume wengine, hujui undani wa maisha ya hao wengine. Ukiishambulia HADHI yake, upendo wake kwako utayeyuka.
5) Usiamiliane vibaya na marafiki wa mumeo kwa sababu tu huwapendi, mtu anayepaswa kuepukana nao ni mumeo.
6) Usisahay kuwa mumeo alikuoa wewe, hakumuoa huyo mfanyakazi wako wa ndani au mtu mwingine. Fanya kutekeleza majukumu yako.
7). Usimpe mtu mwingine jukumu la kumhudumia mumeo. Watu wengine wanaweza kufanya mambo mengine, lakini mumeo ni jukumu lako mwenyewe.
8). Usimshutumu na kumlaumu mumeo akija nyumbani bila kitu. Badala yake mpe hamasa na kumshajiisha.
9). Usiwe mke mbadhirifu, jasho la mumeo ni kitu ghali kabisa ambacho hakipaswi kutupwa hovyo.
10). Usijifanye kuwa unaumwa kwa lengo la kumnyima mumeo tendo la ndoa. Mpe anapotaka. Tendo la ndoa ni muhimu sana kwa wanaume, ni miongoni mwa MAHITAJI MAKUU 3 YA MWANAUME. Ukiendelea kumnyima haitachukua muda mrefu kabla mwanamke mwingine hajachukua jukumu hilo. Hakuna mwanaume anayeweza kuhimili vishindo vya ukame
11). Usimjibu mumeo katika uchangiaji wa maoni ya mbele ya umma, muaje ajibu swali lililoelekeza kwake. Ni muhimu usimpinge hadharani mbele ya watu.
12). Usimfokee au kumpinga mumeo mbele ya watoto. Wanawake wenye hekma na busara hawafanyi hivyo.
13). Usishau kuangalia kama mumeo amependeza na amevaa vizuri kabla hajatoka.
14). Usiruhusu marafiki zako kuwa karibu mno na mumeo.
15). Usiwe na haraka unapokuwa bafuni na unapojipamba. Huko nje mumeo anakutana na wanawake ambao hutumia muda wa kutosha kujipamba.
16).Wazazi, ndugu an marafiki hawana uamuzi wa mwisho kwenye ndoa yako. Usipoteze muda kuwataka wakupe uamuzi wa mwisho.
17). Usijenge upendo wako kwenye pesa na vitu. Kwa sababu ukiwa na pesa nyingi kumzidi hutoweza kumtii na kumheshimu.
18). Usisahau kuwa mumeo anahitaji mtu wa kumakinika naye na mwenye kumsikiliza, usiwe bize sana kiasi cha kutomtilia maanani. Mawasiliano mazuri ndiyo msingi wa kila nyumba yenye furaha.
19). Kama wazo lako limefanya vizuri kuliko la kwake, usifanye ulinganisho wa kujilinganisha naye. Daima mnatakiwa kufanya kazi kama timu.
20). Usiwe mtu wa kumhukumu sana mumeo. Hakuna mwanaume anayempenda mwanamke msumbufu.
21). Mke mvivu huwa na tabia ya kupuuza. Hata hajui kuwa mwili wake unahitaji maji ya kuoga.
22). Je, mume anapenda aina ya chakula unachopika? Jaribu kubadilisha mapishi. Hakuna mwanaume anayefanya mzaha kwenye suala la chakula.
23). Usiwe mtaka makuu kwa mumeo, furahia kila muda na kila kinachopatikana.
24). Ifanye glasi ya maji kuwa ukaribisho nambari 1 kwa mumeo na kila mgeni anayekuja nyumbani kwenu. Mwenendo mzuri ndio urembo wa kweli.
25). Usisuhubiane na wanawake ambao wana mtazamo wa kimakosa kuhusu ndoa.
26). Ndoa yako itakuwa na thamani kadiri unavyoipa thamani. Uzembe haukubaliki.
27). Watoto wako ni baraka kubwa kutoka kwa Mungu, wapende na uwape malezi mazuri.
28). Endelea kutengeneza ushawishi wako ndani ya nyumba yako hata kama una muda mrefu katika ndoa. Usipunguze mapenzi yako kwa familia yako kwa sababu yoyote ile.
30). Mke anayefanya ibada anakuwa amejiimarisha vizuri. Daima muombee mumeo na familia yenu.
Wapo watakaochukia lakini kama umeipenda Like na comment kisha ni follow kila siku

Comments

Popular posts from this blog

VYAKULA MUHIMU ZAIDI KWA MAMA MJAMZITO

LISHE BORA WAKATI WA UJAUZITO NI MUHIMU SANA, KWANI LISHE HII HUTUMIKA KWA MAMA NA MTOTO ANAENDELEA KUKUA TUMBONI. KWA KAWAIDA MAHITAJI YA CHAKULA NA VIRUTUBISHO MWILINI MWA MWANAMKE HUONGEZEKA WAKATI WA UJAUZITO NA KADRI UJAUZITO UNAVYOENDELEA KUKUA, VIRUTUBISHO HIVYO HUTUMIKA KUJENGA MWILI WA MAMA NA MTOTO. HIVYO MAAMUZI YA LISHE AU LISHE MAMA ANAYOPATA HUATHIRI PIA MAENDELEO YA MTOTO ANAYEKUA MWILINI MWAKE. TUTAONA VYAKULA MUHIMU VYA KUZINGATIA LISHE BORA WAKATI WA UJAUZITO NA BAADHI YA VITU VYA KUKWEPA. Mama mjazito akipata mlo wenye mboga za majani Mlo kamili (balanced diet), ni muhimu kwa ajili ya maendeleo mazuri ya afya ya mjamzito na mtoto tumboni. Pamoja na mlo kamili mjamzito hupewa virutubisho ziada (supplements) kwa ajili ya kuongeza madini kama ya chuma na Foliki. Mlo kamili unajumuisha vyakula vya wanga, protini, mafuta, vitamini, madini na maji kama inavyochambuliwa hapa chini; Nafaka na Vyakula vya Wanga. Vyakula hivi huupa mwili nguvu za kufanya kazi iki

UJUE MZUNGUKO WAKO WA HEDHI NA UFAHAMU SIKU ZA KUSHIKA MIMBA

Habari za leo rafiki yangu mpendwa, ni matumaini yangu unaendelea vizuri na kufurahia elimu uipatayo hapa pia napenda kuwapongeza wote wachukuao hatua kwa kutumia virutubisho vyetu na wale wanaouliza pale ambapo hawakupaelewa, hii ni kutokana na maoni yenu juu ya kuwafunza jinsi ya kuweza kuhesabu mzunguko wenu wa hedhi kupanga na kuepuka mimba, leo nipo hapa kuwajuza haya. Sasa basi kutokana na wanawake wengi kutokujua mizunguko yao ya hedhi, hivyo huwawia vigumu kujua ni siku gani iliyosahihi ili akutane na mumewe ama aepuke ili kubeba mimba au kutokushika mimba. Ni muhimu sana mwanamke kujua mzunguko wake wa hedhi, hii pia itakusaidia kujua siku hatari za kushika mimba na vile vile kukusaidia kuepuka mimba usiyoitarajia kwa kutumia kalenda yako kupanga tarehe yako.  NAMNA YA KUHESABU MZUNGUKO WAKO WA HEDHI Ili kujua siku nzuri ya kupata mimba au kuepuka ni lazima kwanza ujue siku ya KILELE BUKUKU (productive/fetal day) kwa maana kwamba ujue siku ambayo huitwa SIKU YA KUMI NA NNE

Here are some tips for you to work for your picnic and barbecue during pregnancy.

1. Understand the foods to avoid during pregnancy: You can still enjoy most foods, but the main summer foods you should avoid include: Uncooked soft cheese, Marinated meat, Homemade mayonnaise, unless it is made with a lion egg cover (shopped mayonnaise is good), Homemade ice cream is made with lion-capped eggs (again, the ice cream bought at the store is good). 2. Check the grilled meat and fish:  It’s perfectly fine to ridicule the burger on the barbecue when you are pregnant, but just check if the meat is cooked thoroughly. Otherwise, you can get food poisoning from bacteria. Check that the meat in the middle is pink and put the skewer in the thickest part of the meat to make sure the juice is clear. And don't worry about offending the owner by checking: it's important when you are pregnant. If you make your own barbecue, wait until the charcoal is red and have a powdery gray surface before you start cooking. Make sure to use separate utensils and plates for raw and coo