Skip to main content

Je unajua kuwa Ndoa Imara Huweza Kutibu Hata Kansa:

Image may contain: one or more people, outdoor and closeup
Maradhi ya kansa yamekuwa yakiwasumbua watu wengi sana kwa nyakati za hivi karibuni. Hata hivyo kuna aina nyingi za kansa, mojawapo ni ile ya kibofu cha mkojo.
Kulingana na utafiti mmoja uliofanywa nchini marekani, imeonesha kwamba, msaada wa karibu unaotolewa na wanandoa kwa wanandoa wenzao ambao, wameathirika na ugonjwa wa kansa ya kibofu cha mkojo, ni aina mojawapo ya tiba inayoweza kuwafanya wagonjwa hao wajisikie vizuri na kuishi kwa muda mrefu.
Utafiti huo ulionyesha kwamba, watu wanaougua ugonjwa huo ambao wako kwenye ndoa, wana nafasi kubwa ya kuishi muda mrefu zaidi ukilinganisha na wenzao ambao hawajaoa au kuolewa. Hali hii haichagui umri, rangi au hata kiwango cha athari ya ugonjwwa wenyewe.
Ndoa Imara Huweza Kutibu Hata Kansa.
Vilevile, tafiti mbalimbali za huko nyuma ziliwahi kuonesha kwamba, ndoa bora na imara zina uwezo wa kuwaongezea ahueni wanandoa wanaougua maradhi ya kansa
ya matiti na ile ya mkojo.
Watafiti hao walizidi kusema kwamba utafiti huo mpya unaweza ukawa na manufaa
zaidi kwa aina nyingine ya kansa. Hali kadhalika utafiti huo ulionesha
kwamba,wagonjwa wa kansa ambao walikuwa wamefiwa na wenzi wao wa ndoa na
wale waliotengana ama kutalikiana, waliathirika na ugonjwa huo zaidi.
Ingawa umri mkubwa nao ulichangia kwa kiwango kikubwa kwenye hali hiyo,
kutokuwa na mpenzi kulionesha wazi kuwa na madhara makubwa.
Sababu hasa, inayoyaofanya kuwa na tofauti hiyo, bado haijaulikani. Hata hivyo,
yapo maelezo machache yanayoweza kutolewa kuhusiana na hali hiyo. Kwa mfano,
mume au mke anaweza kumshauri mwenzi wake amwone mapema daktari, wakati
dalili za mwanzo kabisa za ugonjwa zinapojitokeza. Na pia anaweza kumshauri
mwenzake abadili mwenendo wa tabia zinazoweza kuuongeza madhara
yatokanayo na ugonjwa huu kwa mfano, kuacha kuvuta sigara, kwani tabia ya
uvutaji wa sifara huzidisha kiwango cha ugonjwa huu.
SOMA; Kama Hujui, Ndoa Imara Ni Tamu Kuliko Fedha.
Na pia msaada wa mume au mke, kwa njia moja au nyingine, huzipa nguvu
chembechembe hai za mwili zinazohusika na mfumo mzima wa wa ulinzi.
Uchunguzi huo ulionesha kuwa, wagonjwa wa kansa ya matiti waliokuwa
wameolewa na ambao walihisi kuwa wana uhusiano mzuri na imara na wenzi wao wa ndoa na kuwa wanapewa kila msaada wanaouhitaji, chembechembe zao hai zinazolinda mwili, zilionekana kufanya kazi kwa kiwango cha juu kabisa na hata
ziliweza kuua baadhi ya vijidudu vinavyosababisha ugonjwa huo.
Ndoa bora na imara imekuwa ikitajwa sana kama ni tiba inayoweza kutibu maradhi
mengi ikiwemo kansa na pia imekuwa ikielezwa kwamba, huufanya mwili wa
binadamu kuwa imara zaidi, watu wenye ndoa za mashaka na vurugu, wanapoingia
katika maradhi, wameonekana kudhoofu na pengine kufa haraka, ukilinganisha na
wale ambao wako kwenye ndoa imara.
Kwa hiyo hapa utajua, inaposisitizwa kwamba,wanandoa wajenge ukaribu ambao
utawezesha ndoa zao kuwa bora na imara, siyo tu kwa sababu ya ya kufurahia
mahaba, lakini pia ni kwa sababu ya kunusuru afya ya miili yao. Tafiti nyingi
zimekuwa zikionesha kwamba, wanandoa ambao wako kwenye vurugu za kindoa
hupata madhara mengi ya kimwili, wanawake wanaelezwa kwamba huathiriwa zaidi
na jambo hilo.
Kumbuka huu ni utafiti tu uliofanywa na wenzetu. Nikutakie siku njema na endelea
kujifunza kupitia Raha za chumbani kila siku, ili uweze kuboresha na kubadili maisha yako.
👇👇👇👇👇👇
#Follow Me😘
#Like My Page??
#ShareMy post😘
#Comment Below😘

Comments

Popular posts from this blog

VYAKULA MUHIMU ZAIDI KWA MAMA MJAMZITO

LISHE BORA WAKATI WA UJAUZITO NI MUHIMU SANA, KWANI LISHE HII HUTUMIKA KWA MAMA NA MTOTO ANAENDELEA KUKUA TUMBONI. KWA KAWAIDA MAHITAJI YA CHAKULA NA VIRUTUBISHO MWILINI MWA MWANAMKE HUONGEZEKA WAKATI WA UJAUZITO NA KADRI UJAUZITO UNAVYOENDELEA KUKUA, VIRUTUBISHO HIVYO HUTUMIKA KUJENGA MWILI WA MAMA NA MTOTO. HIVYO MAAMUZI YA LISHE AU LISHE MAMA ANAYOPATA HUATHIRI PIA MAENDELEO YA MTOTO ANAYEKUA MWILINI MWAKE. TUTAONA VYAKULA MUHIMU VYA KUZINGATIA LISHE BORA WAKATI WA UJAUZITO NA BAADHI YA VITU VYA KUKWEPA. Mama mjazito akipata mlo wenye mboga za majani Mlo kamili (balanced diet), ni muhimu kwa ajili ya maendeleo mazuri ya afya ya mjamzito na mtoto tumboni. Pamoja na mlo kamili mjamzito hupewa virutubisho ziada (supplements) kwa ajili ya kuongeza madini kama ya chuma na Foliki. Mlo kamili unajumuisha vyakula vya wanga, protini, mafuta, vitamini, madini na maji kama inavyochambuliwa hapa chini; Nafaka na Vyakula vya Wanga. Vyakula hivi huupa mwili nguvu za kufanya kazi iki

UJUE MZUNGUKO WAKO WA HEDHI NA UFAHAMU SIKU ZA KUSHIKA MIMBA

Habari za leo rafiki yangu mpendwa, ni matumaini yangu unaendelea vizuri na kufurahia elimu uipatayo hapa pia napenda kuwapongeza wote wachukuao hatua kwa kutumia virutubisho vyetu na wale wanaouliza pale ambapo hawakupaelewa, hii ni kutokana na maoni yenu juu ya kuwafunza jinsi ya kuweza kuhesabu mzunguko wenu wa hedhi kupanga na kuepuka mimba, leo nipo hapa kuwajuza haya. Sasa basi kutokana na wanawake wengi kutokujua mizunguko yao ya hedhi, hivyo huwawia vigumu kujua ni siku gani iliyosahihi ili akutane na mumewe ama aepuke ili kubeba mimba au kutokushika mimba. Ni muhimu sana mwanamke kujua mzunguko wake wa hedhi, hii pia itakusaidia kujua siku hatari za kushika mimba na vile vile kukusaidia kuepuka mimba usiyoitarajia kwa kutumia kalenda yako kupanga tarehe yako.  NAMNA YA KUHESABU MZUNGUKO WAKO WA HEDHI Ili kujua siku nzuri ya kupata mimba au kuepuka ni lazima kwanza ujue siku ya KILELE BUKUKU (productive/fetal day) kwa maana kwamba ujue siku ambayo huitwa SIKU YA KUMI NA NNE

Here are some tips for you to work for your picnic and barbecue during pregnancy.

1. Understand the foods to avoid during pregnancy: You can still enjoy most foods, but the main summer foods you should avoid include: Uncooked soft cheese, Marinated meat, Homemade mayonnaise, unless it is made with a lion egg cover (shopped mayonnaise is good), Homemade ice cream is made with lion-capped eggs (again, the ice cream bought at the store is good). 2. Check the grilled meat and fish:  It’s perfectly fine to ridicule the burger on the barbecue when you are pregnant, but just check if the meat is cooked thoroughly. Otherwise, you can get food poisoning from bacteria. Check that the meat in the middle is pink and put the skewer in the thickest part of the meat to make sure the juice is clear. And don't worry about offending the owner by checking: it's important when you are pregnant. If you make your own barbecue, wait until the charcoal is red and have a powdery gray surface before you start cooking. Make sure to use separate utensils and plates for raw and coo