Skip to main content

Posts

MFAHAMU MWANAMKE KIUNDANI NA ANACHOKIPENDA

Recent posts

Je unajua kuwa Ndoa Imara Huweza Kutibu Hata Kansa:

Maradhi ya kansa yamekuwa yakiwasumbua watu wengi sana kwa nyakati za hivi karibuni. Hata hivyo kuna aina nyingi za kansa, mojawapo ni ile ya kibofu cha mkojo. Kulingana na utafiti mmoja uliofanywa nchini marekani, imeonesha kwamba, msaada wa karibu unaotolewa na wanandoa kwa wanandoa wenzao ambao, wameathirika na ugonjwa wa kansa ya kibofu cha mkojo, ni aina mojawapo ya tiba inayoweza kuwafanya wagonjwa hao wajisikie vizuri na kuishi kwa muda mrefu. Utafiti huo ulionyesha kwamba, watu wanaougua ugonjwa huo ambao wako kwenye ndoa, wana nafasi kubwa ya kuishi muda mrefu zaidi ukilinganisha na wenzao ambao hawajaoa au kuolewa. Hali hii haichagui umri, rangi au hata kiwango cha athari ya ugonjwwa wenyewe. Ndoa Imara Huweza Kutibu Hata Kansa. Vilevile, tafiti mbalimbali za huko nyuma ziliwahi kuonesha kwamba, ndoa bora na imara zina uwezo wa kuwaongezea ahueni wanandoa wanaougua maradhi ya kansa ya matiti na ile ya mkojo. Watafiti hao walizidi kusema kwamba utafiti huo mpya unaweza

MKE MWEMA MTU HUPEWA NA BWANA. SIFA ZA MKE MWEMA

SIFA ZA MKE MWEMA 1) Kamwe usinyanyue sauti yako kwa mumeo kwa sababu yoyote ile. Hiyo ni ishara kuwa huna adabu na heshima. Pia niliwahi kufundisha hapa Ndoa Maridhawa kuwa radi haioteshi mazao yetu shambani licha ya kuwa na kelele na sauti kubwa, lakini mvua ambayo haina makelele huotesha mazao yetu shambani. 2) Usitangaze udhaifu wa mumeo kwa familia yako na marafiki zako. Linaweza kukuathiri wewe pia. Wewe ni mtunza siri wa mwenzako, na yeye ni mtunza siri wako. 3) Usitumie mihemko na hisia kali kuwasiliana na mumeo, hujui namna atakavyoitafsiri. Wanawake wenye mihemko iliyopitiliza hawawezi kuwa na ndoa yenye furaha. 4) Usimlinganishe mumeo na wanaume wengine, hujui undani wa maisha ya hao wengine. Ukiishambulia HADHI yake, upendo wake kwako utayeyuka. 5) Usiamiliane vibaya na marafiki wa mumeo kwa sababu tu huwapendi, mtu anayepaswa kuepukana nao ni mumeo. 6) Usisahay kuwa mumeo alikuoa wewe, hakumuoa huyo mfanyakazi wako wa ndani au mtu mwingine. Fany

WANANDOA MPOOO?? NISIKILIZENI KWA MAKINI WANANDOA.

1.UTAMSHANGAA SANA: Mnapooana, hasa baada ya kumpata yule unadhani ni mwenzi halisi na anayekufaa unaamini kwamba utakuwa naye kwa furaha hadi kifo kitakapo watenganisha na utakuwa mtu wa furaha milele. Ila siku moja utaamka asubuhi na kugundua kwamba hata kama ni mtu maarufu sana duniani bado hawezi kukufanya wewe kuwa mtu wa furaha siku zote na zipo siku utakuwa uajiuliza hivi kwa nini ulikuwa na haraka kumkubali na kuoana  naye. Sasa matarajio yanapotea, unajisikia upweke, na unaaanza kujifunza kwamba ndoa si kituo kufikia baada ya maisha ya kujitafutia mtu wa kuishi naye duniani bali safari iliyojaa raha na karaha kuelekea kujuana na kujenga familia bora na imara. 2.UTAFANYA KAZI KUBWA ZAIDI YA ULIVYOTEGEMEA. Mapema watu wanapokwambia ndoa ni kazi unadhani labda itakuwa ni kuvumilia kwa kuwa mwenzako anasahau kufanya wajibu wake katika kazi za kila siku ndani ya nyumba. Na unaamini kwamba hata kama anatabia fulani fulani mbaya basi utamvumilia kwa kuwa unampenda. Kuoana n

JE WAZIJUA SIRI ZA MTINDO WA MAISHA ULETAO AFYA

Hello hellow msomaji wa makala zangu unajua nini...???? Leo nataka nikupe siri za mtindo wa maisha unavyoleta afya njema. Wanadamu ni viumbe kamili. Mara nyingi kile tunachokigawa katika sehemu za kimwili, kiakili, na kiroho ni sehemu za mtu zilizo na uwiano unaoingiliana, wala hazitenganishiki. Kwa maneno mengine, kinachoidhuru akili, kinaudhuru pia mwili. Kwa mfano watafiti wa kisayansi katika uchunguzi wao uliodhibitiwa wamegundua kwamba kicheko kile kitokanacho na furaha na shangwe huleta mabadiliko yanayoweza kupimwa katika mfumo wa kinga mwilini mwa mtu. Unaweza kabisa kuusaidia mwili wako kupigana na ugonjwa kwa vizuri zaidi ukiwa na furaha! Uchunguzi huo huonyesha jinsi akili na mwili vinavyofanya kazi yao kwa pamoja kwa ushirikiano wa karibu sana. Jinsi ulivyo ni kutokana na kile unachokula na unachowaza akilini. Hebu tuchambue kidogo ktk maandiko matakatifu, Katika maelfu ya miaka iliyopita Neno la Mungu lilidokeza kuwapo kwa uhusiano huo wenye nguvu kati ya akili n

Vidokezo 10 vya kufurahia barbeque au pikiniki wakati wa ujauzito

Hapa kuna vidokezo kadhaa vya kufanya pikiniki au BBQ zifanyie kazi wakati ukiwa ni mjamzito 1. Jua ni vyakula vipi vya kuzuia ukiwa mjamzito. Bado unaweza kufurahiya vyakula vingi lakini vyakula muhimu vya msimu wa joto ambavyo unapaswa kujiepusha ni pamoja na: jibini laini lisilopikwa, kuponya nyama, mayonnaise ya nyumbani isipokuwa imetengenezwa na mayai makubwa ya simba (mayonesi iliyonunuliwa duka ni sawa), ice cream ya nyumbani isipokuwa imetengenezwa na mayai makubwa ya simba (tena, barafu-iliyonunuliwa duka ni sawa). 2. Angalia nyama iliyochongwa na samaki . Ni sawa kabisa kumdhihaki Burger kwenye barbeque wakati una mjamzito, lakini angalia ikiwa nyama imepikwa vizuri. Vinginevyo, unaweza kupata sumu ya chakula kutoka kwa bakteria. Angalia kuwa nyama iliyo katikati ni nyekundu na weka skewer kwenye sehemu nene ya nyama ili kuhakikisha juisi iko wazi. Na usijali kuhusu kumkosea mmiliki kwa kuangalia: ni muhimu wakati wewe ni mjamzito. Ikiwa utatengeneza barbeque yako m

LIJUE TATIZO LA KUKOSA CHOO

JE UNALIJUAA TATIZO LA KUKOSA CHOO Tatizo la kukosa choo (CONSTIPATION) ni tatizo ambalo limekuwa likiwakumba watu wengi leo ktk dunia, watu wamekuwa wakiteseka bila kujua nini chanzo cha tatizo hili na vipi kuliondoa tatizo hili na wengine wamekuwa wakilipuuzia bila kujua madhara ambayo wanaweza kuyapata kutokana na tatizo hili.Tatizo hili.Tatizo hili hutokea pale mtu anakula vizuri lakini unakata anakaa siku tatu hadi nne bila kupata choo ukiona unakula kutwa mara tatu na unakaa siku mbili hadi tatu huendi chooni au unatoa choo kigumu kama mbuzi hilo ni tatizo kwako.Tafiti zinaonyesha mtu anaweza kupoteza maisha kama atakosa choo kwa siku tano hadi saba mfululizo.Watu wengi hulidharau tatizo hili lakini linamadhara makubwa tofauti na wanavyofikiria. SABABU ZA KUKOSA CHOO (CONSTIPATION) a) Kupenda kula saana vyakula vilivyokobolewa (mfano ugali wa sembe,mikate n.k) b) Ukosefu wa mbogamboga za majani na matunda ya faiba kama machungwa,ukosefu wa kula mboga za majani na matunda